Tuesday, May 29, 2007

Makumbusho ya Mwalimu Nyerere: Kutoka Nyumba ya Udongo hadi Ikulu

Na Nyasigo Kornel

Huwezi ukasubiri kuambiwa, kwa mara ya kwanza ukifika Mwintongo- Butiama maali alipozaliwa baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere utaona kila hali ya maisha ya mtu wa kawaida na sio kama viongozi wengi wanaojijengea mahekalu na kuweka vizuio katika nyumba zao.

Inawezekana hii pia ikawa imechangia hata kanisa Katoliki kumwona na kumtangaza mwenye heri.

Makumbusho ya Mwalimu N yerere ipo Butiama katika Mkoa wa Mara upande wa kaskazini mwa Tanzania.

Makumbusho haya yalizinduliwa tarehe 2 Julai 1999 na aliyekuwa Waziri Mkuu mheshimiwa Frederick Sumaye.

Butiama ni maali alipozaliwa na ndipo alipozikwa baba wa Taifa Mwalimu J.K Nyerere.

Makumbusho yalianzishwa ili kukusanya, kutunza na kuonyesha vitu vyote ya kitaifa na kimataifa vilivyohusu maisha ya mwalimu J.K Nyerere.

Mwalimu alifariki dunia 14 Octoba 1999 na kuzikwa huko Butiama.

Ukifika Butiama, kuna mambo machache sana yanayoweza kukuthibitishia kuwa kijiji hiki ndicho kilichomzaa na kumlea mwana wa Afrika.

Kutoka katika nyumba iliyojengwa kwa udongo ndipo alipolelewa mtoto aliyeikomboa Tanzania na Afrika katika makucha ya mabepari na mabeberu.

Hakuna uzio kuzunguka kwake, wanawake na watoto huchota maji nje ya huo mji na hata kufua nguo kitu ambacho watu wengi katika ngazi ya Mwalimu wasingekubali.

No comments: