Tuesday, May 29, 2007

Barrick North Mara: Chachu ya maendeleo Tarime


Na Nyasigo Kornel

KABLA ya kuitwa Barrick North Mara ilikuwa ikiitwa East African Gold Mine iliyoanzishwa mwaka 1993 na kupata leseni na kuendesha shughuli za uzalishaji mwaka 1996.

Barrick North Mara waliweka mtambo wao wa kwanza wa uzalishaji 2002 na hapo ndipo mara moja mgozi uliona umuhimu wa kusaidiana na wakazi wa Nyamongo kuboresha maisha yao.

Ili kuhakikisha kuwa wananchi wanaoishi katika maeneo yanayozunguka mgodi wa dhahabu ya Barrick North Mara iliyopo Nyamongo katika Wilaya ya Tarime wananufaika na uchimbaji huo unaoendelea katika eneo hilo, Barrick North Mara imekuwa na shughuli mbalimbali za kuikwamua jamii katika hali ngumu ya kimaisha.

Mgodi wa Barrick imewajenga nyumba za kisasa zipatazo 96 kwa wale waliohamishwa kutoka katika maeneo ambayo uchimbaji unapofanyika. Nyumba hizi ni za kisasa kabisa zinazoweza kukimu familia kubwa.

Baadhi ya wananchi wanaozunguka mgodi huu walipewa zabuni za kujenga nyumba za kisasa kwa ajili ya wanavijiji wanaohamishwa ili kupisha shughuli za migodi.

Hii ilifanyika ili kuwaongezea ajira wakazi wanaozunguka mgodi huo wa North Mara.

Hata hivyo mgodi uliona kuwa sio vema mtu kukaa katika nyumba ya kifahari huku umaskini ukiwa bado unamzingira, na ndipo ulipoanzishwa chama cha kuweka na kukopa cha Mara SACCOS iliyo na wanachama zaidi ya 500 toka kuanzishwa mwaka jana.

SACCOS hii ilipoanzishwa kampuni iliwagharamia baadhi ya wanachama ziara za kwenda kujifunza katika benki zinazofanya kazi chini ya mtandao wa vyama vya kuweka na kukopa nchini maarufu kama Dunduliza Kanda ya Ziwa.

Lengo ilikuwa ni kwamab SACCOS iweze kutoa mikopo ya fedha yenye riba nafuu kwa wanachama wake ili kuwawezesha kuanzisha na kuendeleza miradi ya uzalishaji mali ili kuwaongezea kipato na kupunguza umaskini miongoni mwao.

Kwa ajili ya kuondokana na umaskini wa kipato, mgodi vilevile ulianzisha mpango maalumu wa kuwakopesha wananchi ng’ombe wa kisasa wa maziwa, na kasha mwananchi alitakiwa kulipa ndama wa kwanza na wa tatu tu na kisha ng’ombe wake aliachiwa.

Hii imewaongezea kiwango cha uzalishaji wa maziwa kwa ufugaji uliogharimu malisha ya mbali na hivyo kuboresha utunzaji wa mazingira.

Maziwa yanayopatikana uuzwa Sirari, na mahusianao kati ya Nyamongo na Sirari ni muhimu sana na hivyo mgodi uliamua kujenga barabara kati ya Sirari na Nyamongo kilomita 56 kwa kiwango cha lami.

Katika juhudi za kuinua kiwango cha elimu ya msingi kwa wakazi wa Nyamongo, Barrick North Mara kwa kushirkiana na chuo cha ualimu cha Tarime (TTC) na Halmashauri ya wilaya ya Tarime umeanzisha mpango wa kutoa mafunzo ya kuwanoa waalimu wa shule za msingi zipatazo 24 zilizo jirani na mgodi huo.

Hadi mwaka jana tayari wakuu wa shule 24 na waratibu wa elimu wa kata watano wamekwisha nufaika na mafunzo ya uongozi chini ya mpango huo.

Walimu 64 wa madaraja ya B na C wamekwishapata mafunzo ya wiki tatu ya kuinua taaluma yao yaliyofanyika mwanzoni mwa Aprili mwaka huu, katika chuo cha ualimu Tarime.

Mgodi umewajengea Chuo cha Ualimu cha Tarime (TTC) nyumba ya kuishi mwalimu kama motisha ya mwalimu ili aweze kuishi katika mazingira mazuri zaidi.

Mgodi wa North Mara umetumia mamilioni ya pesa kuongezea majengo ya iliyokuwa kituo cha afya cha Sungusungu hadi kuwa hospitali.

Mgodi umejenga wodi nne za kulaza wagonjwa, jengo la upasuaji na kukiwekea kituo hicho cha afya uzio wa waya.

Kuna msemo usemao kuwa penye wengi kuna mengi, idadi kubwa ya watu katika maeneo yenye makazi ya watu na wafanyakazi kutoka mbalimbali lazima yatakuwa na mwingiliano wa kijamii na kimahusiano.

Hivyo mgodi umeanzisha huduma ya kiafya ya AMREF kinachotoa ushauri nasaa na upimaji wa hiari wa virusi vya UKIMWI kilichopo Nyangoto.

Zaidi ya watu 1600 wamekwishapima kwa hiari virusi vya UKIMWI.

Mgodi umejenga shule ya msingi ya Nyabichune ili kuwasaidia wakazi wa Nyamongo kufikia malengo ya kitaifa katika maendeleo ya elimu.

Vilevile vijana yatima tisa wamepata kufundishwa ushonaji na kupewa darasa maalumu katika ofisi ya mgodi idara ya Maendeleo Endelevu na vyerehani vitatu, vitambaa, uzi na vitabu kadhaa.

Katika uhifadhi wa mazingira, ili kupata dhahabu, mgodi umeamua kutumia cyanide badala ya mekyuri. Mekyuri ina madhara kwa afya ya mwanadamu na mazingira kwa ujumla.

Cyanide hayana athari ya muda mrefu kwa mazingira ukilinganisha na mekyuri kwani yenyewe uyeyuka hewani baada ya kupata joto la kawaida sana.

No comments: